Mauaji ya Kikatili Katika Kijiji Chetu cha Mnini, Uru-East, Moshi Kilimanjaro, Tanzania. Habari kwa Mujibu wa "Global TV Online." Inasikitisha.
Hii ni mbaya sana. Jamii ya #Mnini, #UruEast, #Moshi, #Kilimanjaro, Utu umetutoka kiasi kikubwa sana. *Mungu awaongoze hawa ndugu na awafariji wafiwa.* Jamii ya Mnini imrudie Mungu, iikamate #Adabu, ijenge tabaka la kusimamia #Ukweli, irudie misingi ya #Haki.
Inasemekana hili ni tukio la 3 la Mauaji Kijijini kwetu Mnini. Ni kweli? Matukio ya Kutuchomea nyumba Moto mara mbili kutaka kunwulia Mama yetu Mjane Felicia Moshi, na usimamizi wa kubambikia makesi kila kukicha, hizi nguvu hasi zilizo chochewa na kuvumiliwa na baadhi ya watu/ndugu wanaojulika, tulivyoonya awali, hazidhuru tuu Familia ya Mwl. Valerian na Mwl. Felicia jamani. Uovu na uhalifu, nguvu hasi kwenye jamii, hazina mipaka, rangi, dini, utaufa, tabaka wala kabila.
Pole wafiwa na WanaKijiji cha Mnini. Jamani #Uvunjifu wa utu, na haki za kibinadamu Mnini ni swala linalosikitisha😩 sana. Watu wangu wa #Mnini, pazeni sauti dhidi ya uvunjifu wa utu na haki za binadamu. Usalama wetu ni jukumu letu sote. Hakuna atakaye kuja kutusaidia kurejesha Amani, utu na haki zetu, bila sisi kuanza jitihada leo hii.
Saikolojia ya watu na jamii inatufundisha kuwa jamii ikifumbia macho matendo ya kutokuwa na adabu, utu, haki na ukweli (Uhalifu) wa kuvunja haki za bibadamu, matokeo yake ni makubwa sana. Jamii ya namna hiyo huzorota kiasi kikubwa sana, na huleta maovu mengi kwa wanajamii.
Mfano, viongozi na raia Waliomfumbia macho Hitler, Wahutu, Iddi Amin, Kibwetere, *et la,* walichangia mauaji yaliyotokana na viongozi hawa na wapambe wao. Uchochezi/Violent Incitement ni kitu kibaya sana kwenye jamii yeyote ile. Vionhozi, iwe ni wa familia, Ukoo na Jamii, wakifumbia macho matendo ya uchochezi na kushamiri, matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu hushamiri. Tuamkeni.
Uovu/mauaji hayashamiri bila kudhibitiwa vikali ipasavyo kwenye jamii inayo jenga utu, adabu, kua wakweli na watenda haki. Kwani waovu/wauaji hawapendi mazingira ya adabu, ukweli au haki. Hawapendi kuwajibishwa, ukweli au kutiwa hatiani.
Misingi ya usalama, adabu, ukweli na haki katika jamii ni jukumu la kila mwanajamii. Ila #Uongozi unaovunja hii misingi bayana na kuleta mgawanyiko #Ukivumiliwa, basi na uovu dhidi ya Utu utashamiri.
Wanajamii wapenda utu na haki wakipaza sauti na kupinga uhalifu, hautashamiri. Tuambizane kila mmoja wetu, "tuanze kuilinda jamii yetu." Kwani maendeleo, huzuni, na fura ya mmoja wetu ni yetu sote. Jamani, hatuishi kila mtu kwenye kisiwa chake.
Baba Wa Taifa alionya kuwa tukianza kubaguana/Ukabila (kukosa #Utu) ni sawa na Kula nyama ya Mwadamu, tutaendelea bila kikokomo na tabia hiyo itatapakaa kwenye jamii nzima🤔.
Tutafikia malengo tuu. God help 🆘 us🙏. Go Figure!
No comments:
Post a Comment
Thank you for visiting us🙏🏽. Feel free, be happy, do good/right things & remember that sky is not the limit, but your eyes, dogma & imagination/mind are the only limit. My father, Sr. used to say that the mind is the most powerful resource/thing a human being can ever have; use it wisely. It is similar to a common saying that the mind is a terrible thing to waste.